Gachagua, ODM Waomboleza Aliyekuwa Mbunge Mathew Lempurkel ALIYEKUWA Mbunge wa Laikipia Kaskazini, Mathew Lempurkel , alifariki dunia jana kutokana na majeraha aliyopata ajalini. Bw. Lempurkel alifariki akipokea matibabu katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta (KNH) , baada ya kuhusika kwenye ajali mbaya ya barabarani mwishoni mwa wiki iliyopita eneo la Rongai, Kaunti ya Kajiado. Inaripotiwa kuwa Lempurkel alipata majeraha makali na kulazwa katika Kitengo cha Wagonjwa Mahututi (ICU) , ambako alifariki dunia. Kiongozi wa chama cha Democracy for Citizens Party (DCP) , Bw. Rigathi Gachagua, aliongoza kutoa rambirambi akimtaja marehemu kama kiongozi mwaminifu aliyejitolea kuhudumia umma: “Lempurkel alikuwa mwanachama wa DCP na aliwahi kuwa Mbunge wa Laikipia Kaskazini. Roho yake ipumzike kwa amani ya milele, na Mwenyezi Mungu aipe nguvu, faraja na uvumilivu familia yake, wapendwa wake na wote waliompenda wakati huu wa huzuni. Ameondoka...
Rigathi Gachagua Aapa Kutoa Ushahidi Kuhusu Utawala wa Rais Ruto Aliyekuwa Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua , amejitokeza wazi kuwa yuko tayari kutoa ushahidi kuhusu utawala wa Rais William Ruto , ikiwa ni pamoja na madai ya uhusiano wa kifedha na kisiasa na mataifa kama China, Urusi, na Iran. Gachagua amesema hana hofu ya kuhojiwa kuhusu matamshi aliyoyatoa akiwa Marekani , ambapo alielezea hali ya kisiasa nchini Kenya akisema: "Shida si Kenya, shida ni Ruto." Aidha, Gachagua amekataa wito wa Waziri wa Usalama wa Ndani, Kipchumba Murkomen , kumtaka aandikishe taarifa kuhusu matamshi yake, akisisitiza kuwa hana cha kuomba msamaha. Gachagua amesisitiza kuwa yuko tayari kushirikiana na uchunguzi wowote wa kisheria kutoka kwa vyombo vyote vinavyohusika, ili kufichua ukweli kuhusu uhusiano wa utawala wa Rais Ruto na masuala ya usalama wa ndani na nje ya nchi. Aliiondolewa mamlakani mwezi Oktoba 2024 baada ya kutofautiana na...