Gachagua, ODM Waomboleza Aliyekuwa Mbunge Mathew Lempurkel ALIYEKUWA Mbunge wa Laikipia Kaskazini, Mathew Lempurkel , alifariki dunia jana kutokana na majeraha aliyopata ajalini. Bw. Lempurkel alifariki akipokea matibabu katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta (KNH) , baada ya kuhusika kwenye ajali mbaya ya barabarani mwishoni mwa wiki iliyopita eneo la Rongai, Kaunti ya Kajiado. Inaripotiwa kuwa Lempurkel alipata majeraha makali na kulazwa katika Kitengo cha Wagonjwa Mahututi (ICU) , ambako alifariki dunia. Kiongozi wa chama cha Democracy for Citizens Party (DCP) , Bw. Rigathi Gachagua, aliongoza kutoa rambirambi akimtaja marehemu kama kiongozi mwaminifu aliyejitolea kuhudumia umma: “Lempurkel alikuwa mwanachama wa DCP na aliwahi kuwa Mbunge wa Laikipia Kaskazini. Roho yake ipumzike kwa amani ya milele, na Mwenyezi Mungu aipe nguvu, faraja na uvumilivu familia yake, wapendwa wake na wote waliompenda wakati huu wa huzuni. Ameondoka...